Monday 20 November 2017

TANZANIA YAJITETEA KUHUSU KUPIGA MNADA NG'OMBE WA KENYA



 




Image result for wamasai wakichunga mifugo

Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imesema kupitia taarifa kwamba Tanzania ilifuata utaratibu uliopo kisheria na kwamba mataifa hayo mawili yamekuwa yakiwasiliana.

Waziri wa mambo ya nje nchini Kenya Amina Mohamed ameilalamikia serikali ya Tanzania kufuatia hatua ya taifa hilo.
''Tulidhani kwamba mazungumzo ya kidiplomasia yangetatua mzozo huu, lakini tulishindwa kuafikia makubaliano. Ni wakati huo ambapo tuliamua kuzungumza na balozi wetu nchini humo kuwasilisha barua ya kupinga hatua ya kuwapiga mnada mifugo hao''.
''Historia ambayo tumekuwa nayo na Watanzania ni nzuri sana na kila kunapotokea tatizo tumekuwa tukitatua.Ni kwa sababu hiyo ambapo imekuwa hatua ya kushangaza miongoni mwa wafugaji wa Kenya'', waziri huyo alizungumza katika mkutano na vyombo vya habari.
Wizara ya mambo ya nje ya Tanzania imekiri kwamba Serikali ya Kenya ilimwita balozi wa Tanzania aliyeko Nairobi kutaka maelezo zaidi.
"Balozi wetu alisikiliza maelezo ya Serikali ya Kenya na akatumia fursa hiyo kuelezea masuala haya kwa Serikali ya Kenya. Vile vile Serikali imepokea barua kutoka Serikali ya Kenya kuhusu masuala haya, na Serikali itaijibu barua hiyo kutoa ufafanuzi," taarifa ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki imesema.
"Serikali inapenda kuufahamisha umma kwa ujumla kuwa uingizwaji wa mifugo na bidhaa zake nchini Tanzania huongozwa na sheria za nchi, makubaliano ya kikanda na kimataifa."
Tanzania imesema kuwa ilipobainika kwamba kulikuwa na idadi kubwa ya mifugo kutoka nchi za jirani wameingizwa nchini humo pasipo kufuata sheria na taratibu zilizopo, serikali iliagiza mifugo hiyo irudishwe kwenye nchi kusika.
"Serikali ilitoa muda wa kutosha kwa wamiliki wa mifugo hiyo kuiondoa nchini. Tahadhari ilitolewa kwamba muda uliotengwa ukifikia ukomo, mifugo hiyo itakamatwa na kushugulikiwa kwa mujibu wa sheria za nchi," taarifa hiyo imesema.
Aidha, wizara hiyo imesema Waraka wa Kidiplomasia ulitumwa kwa kwa Serikali za Burundi, Kenya, Rwanda na Uganda, ikizihimiza kuwataka raia wao walioingiza mifugo nchini isivyo halali waiondoe.
"Wamiliki wengi walitii agizo hilo la Serikali ya Tanzania na kuondoa mifugo yao nchini.

No comments:

Post a Comment

KASUMBAI