Saturday 18 November 2017

PENTAGON YASAMBAZA UJUMBE WA KUMTAKA TRUMP AJIUZULU KIMAKOSA

Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResister   
Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @Prou
Ndio idara inayosimamia nambari za siri makombora, Idara inayosimamia usalama wa Marekani na mkuu wake ni rais wa Marekani ambaye hupendelea sana kutumia mtandao wa Twitter.

Lakini inapofikia wakati wa kusimamia akaunti yake ya mtandao huo, the Pentagon inafaa kuimarisha uwezo wake. Siku ya Alhamisi idara hiyo ya ulinzi ilituma ujumbe kimakosa katika mtandao wake wa Twitter ukimtaka rais Trump kujiuzulu.

Ujumbe huo ambao pia uliwataka wanasiasa wengine wawili wa Marekani kujiuzulu kufuatia madai ya unyanyasaji wa kijinsia ulitumwa kutoka kwa akaunti ya @ProudResister, mwanaharakti ambaye ni mkosaji mkuu wa Trump. Akaunti hiyo ilisema: Suluhu ni rahisi. Roy More jiuzulu katika kinyanganyiro. AI: Jiuzulu katika bunge la Congres, Donald Trump Jiuzulu katika urais. GOP: Wacha kulifanya swala la unyanyasaji wa kijinsia kuwa la kibinafsi.Ni uhalifu kama unafiki wao. 

Akaunti ya Idara hiyo ya ulinzi iliusambaza ujumbe huo kimakosa kwa takriban wafuasi wake milioni 5.2 kabla ya kuufuta. Lakini makosa hayo yalionekana. Picha ya ujumbe huo wa Pentagon lisambazwa na majibu yake pia yakawa ya haraka sana.



Ujumbe wa Trump uliosambazwa na akaunti ya idara ya ulinzi ya marekani kimakosa
                                                          

No comments:

Post a Comment

KASUMBAI