Mkufunzi wa klabu ya West Brom Tony
Pulis amefutwa kazi na klabu hiyo huku klabu hiyo ikiwa pointi moja tu
juu ya eneo la kushushwa daraja mbali na kutopata ushindi hata mmoja
katika mechi zake 10 ilizocheza.
West Brom walicharazwa mabao 4 kwa sufuri na mabingwa watetezi wa ligi Chelsea.
Albion
waliwezahinda mechi zake tatu za kwanza msimu huu lakini wameweza
kutoka sare mechi nne na kupoteza saba tangu ilipoishinda Accrington
katika kombe la Carabao 22 mwezi Agosti.
Aliyekuwa mkufunzi wa
zamani wa klabu hiyo Gary Megson ambaye alikuwa naibu wa Pulis anachukua
mahala pake hadi timu hiyo itakapotoa tangazo jingine.
Mwenyekiti
wa klabu hiyo John Williams aliongezea:Uamuzi kama huu hauchukuliwa kwa
urahisi lakini kwa sababu ya maslahi ya klabu.
Tuko katika
biashara ya kupatamatokeo mazuri lkini kutokana na matokeo mabaya ambayo
yamekuwa yakishuhdiwa kufikia mwishoni mwa msimu uliopita na kufikia
sasa matokeo yamekuwa mabaya.
West Brom inakutana na Tottenham ika ligi ya Uingereza katika uwanja wa Wembley siku ya Jumamosi.
No comments:
Post a Comment